MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 17 May 2012

WAZIRI KAGASHEKI ATEUA WAJUMBE WA BODI YA USHAURI;-


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
TAARIFA KWA UMMA
BODI YA USHAURI YA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA (TFS) YATEULIWA
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Balozi Khamisi S. Kagasheki (Mb) kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa Sheria ya Wakala wa Serikali (Executive Agencies Act) Sura 245 amewateua wajumbe saba (7) kuunda Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Tanzania Forest Service - TFS). Aidha, Waziri Kagasheki amemteua Bibi. Ester Mkwizu kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo.
Wajumbe wa Bodi hiyo ya Wakala wa Huduma za Misitu ni kama ifuatavyo:-
1. Bibi. Esther Mkwizu –  Mwenyekiti, kutoka Sekta Binafsi (Tanzania Private Sector Foundation), Dar es Salaam;
2. Bibi. Gladness Mkamba - wa Wizara ya Maliasili na Utalii;
3. Eng. Bonaventura T. Baya –  wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC);
4. Bw. Sosthenes Sambua -  wa Dar es Salaam;
5. Prof. Yonika Ngaga -  wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, Morogoro;
6. Dkt. Himid Majamba -  wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam - Sheria; na
7. Bw. Rawson Yonazi – wa Dar es Salaam.
Uteuzi wa Bodi hiyo ni kwa kipindi cha miaka mitatu (3) tangu tarehe 1 Desemba 2011 hadi 30 Novemba 2014.
George Matiko
MSEMAJI
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
17 Mei 2012

No comments: