MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 29 July 2012

TUME YA TAIFA TA TAKWIMU YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAANDISHI HABARI NCHINI, JUU YA SENSA YA WATU NA MAKAAZI

Afisa uhamasishaji Sensa Makao makuu Bw. Said J. K. Ameir
Ni baada ya kushiriki waandishi wa vyombo binafsi na serikali kutoka mikoa ya kanda ya ziwa na kati ambapo wamejifunza maana ya sense, malengo, faida na jinsi ya kuhesabu ikiwemo kutambua maeneo ya sense.
Awali wakati wa ufunguzi Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Evalist Ndikilo, amesema kuwa sensa ya mwaka huu ina umuhimu wa kipekee kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwani itawezesha kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa malengo ya millennia.
Mkuu huyo wa mkoa ametoa kauli hiyo kwenye ufunguzi wa semina kwa waandishi wa habari kutoka mikoa ya kanda ya ziwa na kati, inayohusu sense ya watu na makaazi, akiwasisitiza kutumia kalamu zao kuwaambia watanzania kujitokeza na kutoa ushiriki wao katika zoezi hilo muhimu litakalofanyika kuanzia usiku wa Agost 26 mwaka huu.
Amesema kuwa ni muhimu kwani raslimali watu ndiyo muhimili wa taifa, hivyo hakuna maendeleo yanayoweza kufikiwa pasipokuwa na uhakika wa idadi ya wakaazi nchini.
Hata hivyo amesisitiza kuwa wananchi wasiwe na shaka wakati wa zoezi hilo, kwani halitaathili shughuli zozote za kijamii, bali kuboresha kwani lengo kuu la sense ni kusaidia kupatikana kwa mipango mizuri ya maendeleo.

Maana ya kufanya sensa nchini ni kukusanya, kuchambua, kutathmini na kuchapisha au kusambaza takwimu za kijamii kuhusiana na watu wote nchini na makaazi yao kwa kipindi maalum.
Sensa kwa waandishi hao wa habari kutoka mikoa ya kanda ya ziwa na mikoa ya kati imewashirikisha waandishi zaidi ya 150 kutoka vyombo binafsi na vya serikali.

No comments: