MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 31 August 2012

WAZIRI MWANRI AFUNGA MKUTANO WA HALMASHAURI 130 KUTOKA MATAIFA YA KENYA, UGANDA, RWANDA, BURUNDI NA TANZANIA

 Pamoja na mambo mengine, waziri wa TAMISEMI amesisitiza matumizi mbadala ya mazingira ili kupunguza uchafuzi wa mazingira na utunzaji wake. Lakini zaidi washirki wameambiwa wakitembea kwenye mikutano kama hiyo wajifunze suala la utawala bora na mazingira, kwani kumekuwepo tabia ya watu kupata fursa za kutembea wakashindwa kujifunza wanabaki kununua nguo na vitu vya kifahari tu.
 Picha juu ni mbunge wa Bukoba vijijini Kason Rwehikiza akimkaribisha Mwanri ili kutoa hotuba ya ufungaji.
 Juu ni mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu FABIEN MASSAWE pamoja na mwenyekiti wa umoja wa halmashauri hizo 130 za ukanda wa ziwa Victoria, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na mshiriki kutoka SNV Mwanza. Na chini ni wananchi akiwemo menejea wa KIROYERA TOURS Wilium Rutta wakifuatilia mada hiyo.
 Chini ni mkuu wa wilaya ya Bukoba ZIPORA LION PANGANI katikati na meya manispaa ya Bukoba Dokta ANATOL AMAN kushoto, pamoja na mshiriki mwingine kutoka Uganda.
 Chini mkurugenzi wa UTT Dokta KIBOLA akihojiwa na waandishi habari kutoka vituo vya redio Kasibante na Vision.
 Dokta KIBOLA akiwa na Matrida Leopord Meneja Redio Vision.

No comments: