Kilichonifanya kufuatilia zaidi ni pale ambapo nimekuta
abiria wanaopumzika kwenye banda hilo la serikali kulazimishwa kulipia shilingi
miamoja za kitanzania ili kujisaidia ndani ya vyoo vilivyopo ndani ya jingo hilo
kwa ajili ya abiria.
Swali langu hapa ni kwanini watu wazima walipie shilingi 400
wakati wa kuingia eneo hilo na pia watakiwe kulipia sh 100 ili wajisaidie?
Kibaya zaidi unapolipia wala hupewi lisiti ya kulipia hiyo
shilingi mia, nilipo dadisi zaidi nilijibiwa lugha ambayo haikunifrahisha,
lakini vijana wanaoonekana pichani ndiyo wanaolipisha na nilipowauliza alipo
bosi wao walisema hawajui alipo wakati lakini wakanitajia jina moja tu la TOM,
je ni haki kulipisha watu paspokutoa stakabadhi?
Nicolaus Mac Ngaiza, nikiwa ndani ya Kivuko cha eneo hili
kiitwacho MV SENGEREMA.
No comments:
Post a Comment