MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 12 December 2012

TETESI ZA USHIRIKINA ZIMEZUA KIZAAZAA MANISPAA YA BUKOBA

Mkuu wa wilaya ya BUKOBA, bi ZIPPORAH  PANGANI, amewatahadharisha Wananchi mkoani KAGERA,  kutojichukulia sheria mkononi,  pale wanapowatuhumu watu kwa makosa mbalimbali.
     Bi PANGANi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, ameonya kuwa hakuna mtu yeyote aliye juu ya sheria,  na kuwa yeyote atakayevunja sheria,  atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.
Mkuu huyo wa wilaya ametoa tahadhari hiyo baada ya kutembelea eneo la Majengo Mapya, Kata KASHAI,  ambapo kundi kubwa la wananchi walikuwa wamekusanyika.
    Aidha, amevitaka Vyombo vya habari kutoa habari zilizohakikiwa kutoka Mamlaka husika.
 Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani KAGERA, Mrakibu Mwandamizi wa polisi – SSP  RICHARD   NGOLE, amesema kuwa Watuhumiwa Sita wanashikiliwa na jeshi la polisi,  kuhusiana na tukio hilo.
   Mtuhumiwa huyo, ambaye ni mwanamke,  amelazimika kupelekwa polisi, baada ya watu wenye hasira  kuingia ndani ya nyumba yake,  kufuatia kuwepo uvumi  kuwa alikuwa anawahifadhi watoto  sita,  kwa lengo la kuwafanyia vitendo vinavyodaiwa kuwa ni vya ushirikina.
 Polisi wakipiga mabomu ya machozi ili kutawanya mamia ya raia waliotaka kuvunjwa nyumba ya mtuhumiwa huyo.
 Wanamgambo na askari polisi wakikusanya baadhi ya raia wanaosadikiwa kusha mawe katika vurugu hizo



Katika vurugu hizo, raia mmoja ambaye picha yake haikuwekwa hapa, ameripukiwa na bomu hilo na kumsababishia maumivu makali usoni na mikononi kupasuliwa vidole.

No comments: