MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 29 April 2013

MKUU WA MKOA WA KAGERA AMEOMBA USHIRIKIANO KWA VYOMBO VYA HABARI KUHAMASISHA KUHUSU SIKU YA MASHUJAA 2013

Mkuu wa mkoa wa KAGERA, Kanali mstaafu FABIAN MASSAWE, ameshauri vyombo vya habari na Wana habari kuhamasisha jamii mkoani humo kujiandaa kikamilifu  kwa ajili ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa.
Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa  hufanyika  kila tarehe 25 mwezi Julai. Kitaifa mwaka huu  yatafanyika Julai 25, mkoani KAGERA, katika kambi ya Jeshi la Wananchi-JWTZ-KABOYA, wilayani MULEBA.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo  atakuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk JAKAYA KIKWETE.

Kanali MASSAWE amesema  vyombo vya habari na Wanahabari  ni kiungo muhimu katika kuhamasisha jamii iweze kushiriki kikamilifu katika maadhimisho hayo.

Ameshauri Wazee walioshiriki matukio  wakati ule kujitokeza na kusimulia  ili liwe fundisho kwa   jamii ya sasa itambue uzalemdo wa kuipigania nchi yao.

Aidha, amewataka Wakazi wa mkoa wa KAGERA kutumia fursa hiyo kuwekeza zaidi na kupata ajira.
 Picha juu na nichi ni baadhi ya waandishi habari wa vyombo mbalimbali wakifuatilia katika mkutano huo uliowashirikisha wadau wa habari pia.
MWANA HARAKATI

No comments: