MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 4 August 2013

BAADA YA HALMASHAURI KUZINDULIWA NA KUGAWANA WAFANYAKAZI, WANANCHI WAZUNGUMZA

Wananchi wilayani Kyerwa mkoani Kagera, wamesema kuwa wamesubiri utekelezaji wa viongozi kuwa tayari wameshajitenga kutoka Karagwe, hivyo viongozi waliopangiwa huko watekeleze kazi zao kwakufuata maadili na sheria za nchi.

Wamesisitiza kuwa bado wanakabiliwa na suala la miundombinu, ambayo hatahivyo ni pamoja na barabara, zahanati, umeme na maji, ambavyo bila kupatikana kwake haitaweza kuendelea kama halmashauri zingine.

Katika upande mwingine, wapo wananchi wanaomlalamikia mbunge wa jimbo hilo kuwa tangu ameingia madarakani hajawai kutembelea eneo hilo hadi alipofika rais, na pia amejenga shule kwenye eneo alilopenda yeye, wakinukuu kama hakuwalenga wananchi bali ni kwa maslahi binafsi.

MWANA HARAKATI

No comments: