MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 2 February 2014

MAN U JAMANI!!!!!!!!!!

Katikati Charlie Adam akishangilia na Mark Hughes baada ya kufunga mabao mawili yaliyoifanya Stoke imalize ukame wa ushindi ndani ya mechi sita.

MABAO mawili ya Charlie Adam yameipa Stoke City ushindi wa kwanza kabisa kihistoria dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Britannia.

Adam alifunga mabao hayo dakika ya 38 na 52, wakati bao pekee la United lililofungwa dakika ya 47 na Robin van Persie.

Kiungo mpya wa United, Juan Mata alicheza kwa dakika zote 90 na hakuweza kuwaepusha Mashetani hao Wekundu na kipigo. United sasa inabaki na pointi 40 baada ya kucheza mechi 24 na inaporomoka hadi nafasi ya saba kutoka ya sita.
MWANA HARAKATI

No comments: