Kamanda wa kikosi cha amani cha Umoja wa Afrika katika Jamhuri ya
Afrika ya Kati anasema askari wake wameukomboa mji wa Sibut, kutoka kwa
wapiganaji wa zamani wa Seleka.
Wapiganaji wa zamani wa Seleka - wengi wao Waislamu - wamekuwa wakiondoka mji mkuu, Bangui, ambao uko kama kilomita 200 kusini ya Sibut.
Kuondoka kwa Seleka kumezusha mauaji ya kulipiza kisasi, na watu zaidi ya 40 wameuwawa mjini Bangui katika siku chache zilizopita.
Uchaguzi mkuu ncini Thailand umeanza leo huku ilinzi ukiwa umedhibitiwa, na kukiwa na taarifa za vurugu katika baadhi ya maeneo.
Umoja wa mataifa unakadiria kwamba takriban watu millioni 3.7 nchini Sudan kusini
wanakabiliwa na uhaba wa chakula kutokana na mapigano kati ya vikosi vya
serikali na waasi walio watiifu kwa aliyekuwa makamu wa Rais Riek Machar.
No comments:
Post a Comment