MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 23 March 2014

MAAJABU;PADRI ATOA TUNGULI KABURI LA NGWEHA

Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Monica, Kihonda mkoani Morogoro, Octavian Msimbe akionyesha tunguli zilizozungushiwa sanda zilizokutwa kaburini kwa marehemu Ngwea.
 

Wakati hati ya kifo cha aliyekuwa rapa bora Bongo, marehemu Albert Keneth Mangweha ‘Ngwea’, ikiendelea kushikiliwa nchini Afrika Kusini alikokutwa na umauti mwaka jana, kwenye kaburi lake kumekutwa tunguli zilizozungushiwa sanda.

Tunguli hizo zilikutwa Ijumaa ya wiki iliyopita na Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Monica, Kihonda mkoani Morogoro, Octavian Msimbe ambapo ziliibua hofu miongoni mwa waumini wa kanisa hilo lililopo katika eneo hilo la makaburi.

Awali, ilielezwa kuwa siku hiyo padri huyo alioteshwa ndoto usiku juu ya uwepo wa vitu vya ajabu katika makaburi hayo ndipo akakemea kabla ya kwenda kuvishuhudia asubuhi yake (Ijumaa iliyopita) huku paparazi wetu akinyetishiwa na kuwahi eneo la tukio.

Alipoombwa kutaja majina ya waumini hao alisema: “Sitaweza kutaja majina yao wala ya kigango yaliyoandikwa kwani wanajijua wenyewe na mbaya zaidi hata waumini wataona katika ibada Jumapili hii (Jumapili iliyopita), nitaonesha madhabahuni,” alisema padri huyo ambaye tangu alipofika kwenye kanisani hilo limekuwa na maendeleo makubwa.


Stori: Dustan Shekidele
Na Mwanaharakati.

No comments: