|
|
| Sehemu ya uzio unaozunguka eneo likalojengwa Hospitali mpya ya rufaa mkoani Mtwara. |
“Mradi
wa hospitali ya Rufaa ya Mtwara umelenga kutoa huduma za rufaa kwa kanda ya kusini
hususan mikoa ya Mtwara, Lindi, na Ruvuma, hospitali hii itakapokamilika
inategemewa kuchukua wagonjwa wa nje na ndani watakaohudumiwa kwenye vitengo
mbalimbali vinavyojitosheleza kwa vifaa na wataalamu, “ alisema Dkt. Maarifa.
Kwa
mujibu wa taarifa za awali mradi ulianza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2012/13
kwa fedha za Serikali zinazotolewa kupitia ngazi ya wizara ambapo mpaka sasa
ujenzi wa uzio kuzunguka eneo hilo umekamilika.
Akizungumza
wakati wa ziara hiyo, mmoja wa viongozi wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo
kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri alisema kuwa serikali inatambua umuhimu wa
suala la afya kwa wakazi wa mikoa ya kusini, na akatoa wito kwa uongozi wa mkoa
kuzingatia na kusimamia matumizi sahihi ya fedha za serikali katika mradi huo.
Serikali
imeaandaa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano ukiwa na lengo la kuwa na mfumo
madhubuti wa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025. Lengo la Dira ni kuibadili Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa
kati ifikapo mwaka 2025.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment