![]() |
| Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo waandishi na wahariri kutoka vyombo mbalimbali nchini. |
Akifungua warsha ya siku moja kwa waandishi wa habari kuhusu nafasi ya watetezi wa haki za binadamu na asasi za kirai katika katiba mpya jijini Dodoma, Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe Samia Sululu Hassan amesema waandishi wa habari wana nafasi kubwa ya kuelimisha jamii juu ya haki za binadamu kupitia kalamu zao kwa kuzingatia weledi wa fani yao na maadili ya uandishi.
“waandishi wa habari pamoja na wahariri wao wanaweza kwa kuweka mbele maslahi ya taifa kuripoti na kuandika habari zenye kuleta suluhu, amani, mshikamano na utulivu,” amesema.
Amesema waandishi wa habari kwa kutumia kalamu zao wanaweza kushauri
na kushirikiana na serikali na mamlaka zingine kupatikana kwa katiba mpya yenye
tunu za taifa,
Amesema kwamba kupitia bunge la katiba wanahabari ni kiungo muhimu
katika kufikisha ujumbe kwa wananchi na kuelimisha umma jinsi sheria na haki za
binadamu zinavyoweza kulinda na katiba ya nchi.
Olengurumwa aliongeza kwamba rasimu ya katiba pia haijatambua wasaidizi wa kisheria wakujitolea (Paralegal) ambao wanatoa msaada mkubwa kisheria kwenye ngazi za vijijini.
Amesema ni muhimu kwa watanzania kuendelea kupanua mjadala wa katiba ili misingi ya haki za binadamu iingie kwenye mifumo ya utetezi wa haki za binadamu nchini.
Olengurumwa amesema waandishi wa habari kama vile watetezi wa haki za binadamu maisha yao lazima yalindwe na kutetewa na katiba ya nchi ili kujenga mazingira mazuri ya haki za binadamu nchini.
Hivi karibuni rasimu ya pili ya Katiba ilipendekeza Muungano wa Serikali tatu – Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Tanganyika.
Mjadala wake ulianza, ambapo wasomi walikosoa takwimu za Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuhusu idadi ya waliotoa maoni, kuwa zimetumika kuupotosha umma.
wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Sabato Nyamsenda na Bashiru Ally wakati wakizungumza katika kipindi cha Je, Tutafika? kinachorushwa na Channel Ten hivi karibuni.
Na Mwanaharakati.



No comments:
Post a Comment