MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 24 April 2014

ANALOJIA KUZIMWA APRIL 30 2014 MKOANI KAGERA


Kulia ni Mery Msuya katibu TCRA, Frederick Ntobi kaimu TCRA, Lawi Odielo meneja kanda ya ziwa na kushoto ni Jasson Ndanguzi kutoka wizara ya mawasiliano sayansi na teknolojia.
Injinia Lawo Odielo akifafanua jambo kwa wanahabari.
Baadhi ya wanahabari Kagera wakifuatilia kwa karibu

Moja ya aina ya King'amuzi ikioneshwa utendaji wake kwa wanahabari
Picha ya pamoja


Amesema kwa sasa timu nzima ya taifa katika utoaji elimu kwa UMMA kuhusu mabadiliko ya teknolojia ya mawasiliano nchini, ipo mkoani Kagera ikitoa elimu jinsi ya wananchi kukabiliana na mabadiliko hayo.

Sambamba na hilo, wameshirikisha wadau wa matangazo zikiwamo redio zilizoko kwenye eneo husika, na matangazo kwa njia ya gari ambayo yatakuwa yakipita katika mitaa ya Bukoba kwa ajili ya taarifa hiyo.

Katika mabadiliko hayo, matangazo ya Digitali yatasambaa kilomita 80 katika eneo husika, ambapo maeneo ya Karagwe yanaweza kupata kwa kuweka Dish au Antenna nje kulingana na king’amuzi kitakachokuwa kimenunuliwa na mteja.

Bwana Ntobi, amesisitiza kuwa wanaotumia dishi binafsi na Cable hawataathirika baada ya mitambo yao kuzimwa, huku akisema kuwa waliokuwa wakipata TBC kwa njia ya Antenna hao hawataipata kabisa.

Na Mwanaharakati.

No comments: