MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 18 April 2014

ASKOFU KILAINI AITAKA JAMII KUOMBEA VIONGOZI NGAZI YA MTAA HADI TAIFA KATIKA IBAADA YA IJUMAA KUU BUKOBA

Baadhi ya waumini wakitoka katika kanisa la MATER MIZEL COMBDIEL mjini Bukoba.

Hayo yamesemwa na baba askofu msaidizi jimbo katoliki la Bukoba, muhasham METHODIUS KILAINI, katika ibaada ya ijumaa kuu, kama kumbukumbu ya mateso ya Yesu Kristo.
Baba askofu Kilaini, amesema kuwa ni siku ya kumwomba mungu atuhepushe na majanga na uchochezi, huku akisistiza kuwa jamii ipinge na kukomesha wenye kuwarubuni, kubaka watoto na kuua albino kwa tama ya fedha.
Katika ibaada hiyo, askofu Kilaini amehimiza kuwaombea wenye madhambi hayo kutubu, na kama hawatamrudia Mungu wataendelea kupata matatizo yasiyozuilika, huku akiwataka waumini kuwaombea viongozi wote kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa, pamoja na mchakato wa katiba.

Amesema kuwa maagizo ya mwenyezi Mungu, yanatuelekeza kuacha kuwadanganya wasiojiweza, na yatima ili tuongoke, na kuacha kutapeli  mali za wanyonge kwa kufisadi mabilioni ya fedha huku wakila chakula cha kawaida kama wengine, hali ambayo amesema kuwa ni uonevu kwa wasiojiweza.

Ibaada ya ijumaa kuu husaliwa kote duniani, ambapo wakristo hukumbuka mateso ya Yesu Kristo, hivyo waumini hutumia nafasi hiyo kupinga matendo ya Yuda ambaye hakushiba mpaka alipojitundika.

Na Mwanaharakati.

No comments: