MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 30 April 2014

UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE KUZIMA MAADHIMISHO YA UHURU WA HABARI

Waziri Mkangara
Katika maelezo ya Mh waziri kuhusu uzinduzi wa mbio za mwenge, amesema kuwa hasa vijana watumie mwenge huo kudumisha amani upendo na mshikamano, na kuongeza kuwa mbio hizo za mwenge wa uhuru zitafikia kilele chake tarehe 14 oct 2014 mkoani Tabora.
Kulia ni mkuu wa mkoa wa Kagera Mh Fabian Massawe, akifafanua jambo kwa wanahabari.
 Kaulimbiu ya mbio za mwenge 2014, ni "jitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba mpya"
 Katika mbio hizo za mwenge utazunguka na kufikia halmashauri/manispaa 165 za jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo mwaka jana ulizindua miradi yenye thamani ya zaidi ya bilioni 184 na milioni 578 na laki 6.
Hawa ni baadhi ya waandishi habari wakifuatilia kwa karibu


Siku ya uhuru wa habari, uhadhimishwa May2 kila mwaka, ambapo kwa waandishi habari huweza kuzungumzia uhuru wa kazi zao za kihabari, pamoja na kuzungumzia masuala yanayowakabili wanahabari na kazi zao katika maeneo ya kazi.

Kutokana na siku hiyo muhimu, waandishi habari wameona watumie nafasi hiyo kujua mikakati ya wizara yao kuhusu utekelezaji wa shughuli za kihabari, wizara inazungumziaje siku hiyo na kauli mbiu ya mwaka huu pamoja na kuzungumzia nafasi ya vyombo vya habari na wanahabari katika suala la upatikanaji wa katiba mpya, ila kwa Kagera wamegonga mwamba kuzungumza na waziri, ilhali na naibu wake Juma Suleiman Nkamia naye akiwa Kagera katika mikakati hiyohiyo ya mwenge.
Na Mwanaharakati.

No comments: