MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 30 April 2014

KUSHUKA KWA KIWANGO CHA ELIMU KAGERA HIKI HAPA



Wanafunzi wa Kidato cha Tano na sita, katika Shule ya Sekondari ya Lukole, iliyopo wilayani Ngara mkoani Kagera wanalazimika kutembea umbali wa kilomita saba kufuata huduma ya maji, kutokana na kuharibika kwa mashine ya kusukuma maji.

Akisoma risala kwa niaba ya wanafunzi hao, wakati wa mahafali ya nne ya kidato cha sita, Ishengoma Edibily amesema kuwa kutokana na kuharibika kwa mashine hiyo, inayosimamiwa na idara ya maji, wanalazimika kukatisha baadhi ya masomo.

Ishengoma amesema kuwa, hali hiyo inawaathiri Kitaalaum kutokana na kutumia muda wingi wa kujifunza kutafuta maji.

Amesema kuwa mbali na shule hiyo kukabiliwa na ukosefu wa huduma ya maji, pia inakabiliwa na ukosefu nishati ya umeme na upungufu wa vitabu kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia masomo.

Akizungumza katika mahafali hayo, Mkuu wa wilaya ya Ngara Bwana Costantine Kanyasu amesema kuwa, wananchi wa eneo la K9 wataondokana na tatizo la ukosefu wa maji baada ya kufungwa mashine na nishati ya umeme.

Bwana Kanyasu amesema kuwa, halmashauri ya wilaya ya Ngara tayari imepokea zaidi ya Shilingi milioni 80 kutoka Ofisi ya Rais, na kuwa mashine itakayofungwa katika chanzo cha maji cha K9 itasaidia kuwapatia maji wakazi wa eneo hilo.
Na Mwanaharakati.

No comments: