Ni raia wa Burundi wamekamatwa mkoani kagera wakati wakijiandaa kusafiri kuelekea nchini Burundi na kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu mkoani Kigoma.
![]() |
| Kamishna msaidizi George Kombe akizungumza na waandishi wa habari. |
![]() |
| Ni baadhi ya wahamiaji haramu wakizungumza na Kamishna msaidizi wa Magereza. |
Akizungumza na waandishi wa habari kamishna msaidizi mkoani Kagera George Kombe, amesema kukamatwa kwa wahamiaji hao haramu kumefuatia taarifa zilizotolewa kwa idara hiyo kutoka kwa raia wema.
Amesema wahamiaji hao walikamatwa April 16, 2014
wakiwa wamepakiwa kwenye gari aina ya Toyota
AICE lenye nambari za usajiri T 633 CPZ lilowasafirisha kutoka eneo la Mtukura mpakani wa Tanzania na Uganda.
![]() |
| Gari iliyokuwa imewabeba wahamiaji hao |
KOMBE amesema taratibu za kuwasafirisha watuhumiwa
hao zilikuwa zimekamilika na kueleza kuwa, ilikuwa wasafirishwe kuelekea maeneo
ya mpaka wa Burundi mkoani kigoma.
Awali baadhi ya wakimbizi hao wamedai kuondoka
pasipo kuaga katika kambi ya wakimbizi ya nchini Uganda wakidai kuwa maisha
katika kambi hiyo yamekuwa magumu.
Wanasema kuwa wakimbizi katika kambi hiyo wanakabiliwa
na tatizo la ukosefu wa kuni,maji, na chakula, huku wakilalamika kuwa misaada
inayotolewa na mashirika mbalimbali ili kusaidia kambi za wakimbizi kwa kiasi
kikubwa haziwafikii walengwa.
Wahamiaji hao wametokea kambi ya Nyakivala nchini Uganda wakielekea Nyalugusu, baada ya kupata taarifa kuwa wakimbizi wa pale wamepata fursa ya kwenda kuishi Uingereza, wengine walitaka kwenda Burundi baada ya kukosa huduma sahihi katika kambi ya Nyakivala.
Na Mwanaharakati.



No comments:
Post a Comment