MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 20 May 2014

NEWS ALERT!!! WAWILI WAUAWA NA TEMBO BAADA YA KUVAMIA MAENEO YA WATU

Jumla ya Tembo nane wamevamia kata ya mpunguzi Mkoani Dodoma na kusababisha vifo vya watu wawili pamoja na uharibifu wa mali.



Akitoa taarifa hii kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma  David Misime amesema kuwa mnamo tarehe 18/5/04 majira ya saa kumi jioni katika kitongoji cha mkwawa Kata ya mpunguzi  Jofrey  Mkalabure  ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi.

 Mpunguzi  alikanyagwa na tembo  waliovamia kitongoji hicho na kumsababishia mauti.
Aidha Kamanda Misime amesema  Tembo hao walimvamia Bi. Elizabet Mgawa mwenye umri wa miaka 89 na kumsababishia majeraha  mbalimbali katika sehemu zake za  mwili  na punde baada ya kupelekwa hospital ya mkoa wa Dodoma kwa ajili ya matibabu alifariki.  

Kamanda Misime ameongeza kuwa katika tukio hilo jumla ya watu watano wamejeruhiwa ambapo wote wametibiwa na kuruhusiwa.

Kamanda wa polisi ametoa wito kwa wananchi  kushirikiana na jeshi la polisi  pamoja na idara ya wanyama pori kwa kutoa taarifa pindi watakapowaona tembo hao na kutokuwafuata tembo hao wala kuwapigia kelele.
  Na Mwanaharakati.

No comments: