MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 8 May 2014

NEWS ALERT!!!HOMA YA DENGUE YAMKUMBA MSANII MWINGINE





Msanii wa filamu nchini, Dr Cheni amelazwa toka jana katika hospitali ya Buruhani jijini Dar es Salaam kutokana na ugonjwa wa Dengue.

Akizungumza na waliomtembelea, amesema kuwa bado hali yake sio nzuri kutokana na kuishiwa damu na mwili kupoteza nguvu.
 
“Bado ni nipo hospitali ya Buruhani naumwa hili gonjwa jipya,sijui unaitwa Dengue,” amesema. “Bado hali yangu sio nzuri kabisa,yaani naumwa, napungukiwa damu, mwili unauma, kwahiyo bado ninaumwa, hii homa ilinianzia wiki iliyopita sema ilikuwa bado hawajaigundua ila jana ndio wameingundua,” ameongeza.
 
Dr Cheni amesema kuwa anawaomba Watanzania wamuombee kwani bado hali yake sio nzuri.
Na Mwanaharakati.

No comments: