MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 24 May 2014

NEWS ALERT!!!VIFO VYA WATU MULEBA; AHADI YA POLISI ITIMIZWE

Ni baada ya kuahidi kujenga kituo katika kata Muhutwe mwaka jana na hawajafanya hivyo.
RPC KAGERA- MAYUNGA
 Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera GEORGE MAYUNGA ameagiza waganga wote wilayani muleba wasakwe na kukaguliwa vibali vyao.

Kamanda MAYUNGA  amesema hayo Siku moja baada ya mganga wa kienyeji kukamatwa na jeshi la polisi na kukiri kuhusika na tukio la mauaji ya mtoto wa miaka nane.
MGANGA ANAYTUHUMIWA
Kamada MAYUNGA amemuagiza mkuu wa kituo cha polisi muleba kuhakikisha ndani ya muda mfupi ambao hakuutaja  kuhakikisha wanabainisha ni waganga wangapi waliopo wilaya ya Muleba na niwangapi wanapiga lamuli za uchonganishi kama alivyokuwa anafanya mganga huyo aliyekamatwa.

Ameongeza kuwa waganga wanaopiga lamuri ni wachonganishi ndio  wanaochochea vurugu katika jamii ikiwa ni pamoja na kusababisha mauaji ya watu wakiwemo maalubino, vikongwe na watoto.
ALIYEKUWA RPC KAGERA- KALANGI
Mapema mwaka jana kupitia vipindi vya redio, mwandishi Mac Ngaiza, alifanya uchunguzi kuhusu vifo vya watu ambavyo vimefuata pasipokujulikana muuaji wake ambapo mpaka nafanya vipindi hivyo vifo vyenye utata vilishazidi 6 kwa mwaka mmoja.

Aliyekuwa kamanda wa polisi mkoani Kagera wakati huo Philp Kalangi pichani, aliahidi kuweka kituo cha polisi katika eneo hilo, kutokana na wananchi kuwa walikuwa wameshaamua kuwa wanajifungia mapema kabla ya saa moja kutokana na vifo hivyo vya kutekwa kuchinjwa na kuchunwa ngozi.

Hivyo wakati kandayaziwa blog ikiendelea kufuatilia, itajikita zaidi kujua kwanini ahadi ya polisi haitekelezwi ilhali vifo vikiendelea.
Na Mwanaharakati.

No comments: