MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 21 May 2014

NEWS ALERT!!!WATU 118 WAMEUAWA KWA BOMU


 Mabomu mawili yalilipuka mojawepo ikiwa imefichwa ndani ya gari na kulipuka katika soko moja kubwa. Dakika 20 baadaye mlipuko wa pili ulitokea karibu na hospitali.


Inahofiwa kuwa kuna maiti zaidi zilizonaswa kwenye vifusi vya majengo yaliyo poromoka kutokana na shambulio hilo.



Kufikia sasa hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulio hilo lakini wengi wanaamini kuwa Kundi la wapiganaji wa kiislamu la Boko Haram lilihusika.

Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amejitokeza kukemea mashambulio hayo na kusema kuwa amejitolea kuangamiza kabisa ugaidi.

Mji wa Jos unatazamiwa kuwa mji mkuu wa jimbo la Plateau ambalo liko katika eneo la katikati linalo tenganisha kaskazini iliyo na raia wengi zaidi wa kiislamu, na kusini lililojaa wakristu zaidi.
Na Mwanaharakati.

No comments: