MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 6 May 2014

TANKI LA MAFUTA LIMELIPUKA SINGIDA NA KUSABABISHA ADHA KWA WATUMIAJI WA BARABARA




Msururu wa magari ukiwa mkubwa katika eneo hilo na  wasafiri mbalimbali wakitoka kuangalia tukio hilo baada ya kushindwa kupita kutokana na moto mkubwa uliokuwa ukiwaka.


Lililipuka majira ya Saa 11:00 katika barabara kuu ya Dodoma Mwanza eneo la Shelui mkoani Singida, wakati breki za tanki hilo upande wa kushoto zilipojam na kusababisha moto, na kumsababishia dereva wa lori lenye namba za usajiri T 164 CGF aina ya Scania lililokuwa likivuta tanki hilo kusimamishwa na kukata haraka tanki hilo huku akiondoa haraka injini ili kuepusha madhara zaidi ambayo yangeweza kutokea.

Tukio hilo lilisababisha usumbufu mkubwa kwa abiria na msururu wa magari kushindwa kupita katika eneo hilo, kutokana na moto mkubwa uliochanganyika na moshi kutishia usalama wa watumiaji wengine, hata hivyo baada ya moto kupungua askari wa usalama barabarani waliamuru magari yaanze kupitia pembeni mwa barabara hiyo ili kuendelea na safari hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa katika tukio hilo.
  Na Mwanaharakati.

No comments: