MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 9 June 2014

KANISA LA SABATO ARUSHA LIMETOA MSAADA KWA WAHANGA WA MAFURIKO THEMI YA SIMBA




 Akikabidhi chakula hicho, mzee wa kanisa la Waadventista wasabato  mtaa wa Kijenge   Agrey Tumaini, alisema kuwa wameamua kuwasaidia wananchi hawa kutokana na janga la mafuriko ya maji  ambapo yaliwasababishia nyumbakuezuliwa  pamoja na mazao yao kusombwa  na maji hayo

Alisema kuwa wao kama kikundi cha WAMO  kutoka katika kanisa hilo waliguswa sana na tatizo hili hivyo wakaamua kujichanga na kununua vyakula ivyo na nguo kwa ajili ya wahanga hao wa mafuriko.

Alisema kuwa wameweza kutoa gunia kumi za mahindi ,maharage kunia tatu,unga wa ugali pamoja na nguo kwa ajili ya watoto  wa wananchi ambao walikubwa na janga hilila mafuriko.
 
Akipokea msaada huo, mmoja wa wananchi hao alietambulika kwa jina la  Gidion Maganga, alishukuru kwaniaba ya jamii yao na kuongeza kuwa baadhi yao walikuwa hawajui hatima ya maisha yao kwani ata chakula kwao kupata ni tabu .
Alisema kuwa pamoja kuwa kuna baadhi yaviongozi na taasisi ambazo zimewapelekea chakula kama maindi ,magodoro  pamoja na nguo, bado wanaitaji msaada, kwani mvua zile ziliwachukulia vitu vyao vingi ikiwemo mazao maindi waliokuwa wameyaifadhi ndani vyombo ,magodoro na sio ivyo tu lakini pia zileweza kumuua mwananchi mmoja.

Alitoa wito kwa wananchi serekali pamoja na taasisi mbalimbali kujitokeza kwa wingi kuwasiaidia kwani wapo katika halingumu sana  katika kipindi hichi.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: