MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 29 June 2014

MISS GEITA 2014; AIBUKA RECHAL KWILA




SHINDANO la kumpata mrembo wa mkoa wa Geita, Miss  Redds Geita 2014 limefikia tamati kwa Recho Kwila kuibuka mshindi wa Taji hilo.

Shindano hilo lililofanyika katika ukumbi Disire  mkoani humo kwa kuwashilikisha walimbwende 11 kutoka wilaya za mkoa wa Geita, lengo kubwa likiwa niku mpata mlibwende wa kuuwakilisha mkoa wa Geita.

Akizungumza katika Tamasha hilo, mgeni rasimi ambaye ni kaimu mkuu wa mkoa wa Geita Omari Manzie Magochie, aliwataka wazazi na walezi kuwaachia watoto wao kujiunga ulimbwende kwani si huuni kama wanavyo fikilia na kusema  ni kazi kama kazi Nyingine.

Naye mshindi huyo akizungumza baada ya kupata taji hilo, alisema kuwa yeye atajitaidi kuwasaidia watoto wanao wa mitaani, na kutangaza Vivutio  vilivyopo katika mkoa wa Geita kikiwemo kisiwa cha Rubondo  na Madini,  ili wageni  wanaokuja wajue kilichopo katika mkoa huo.

 Na Mwanaharakati.

No comments: