
![]() |
Katibu mwenezi kushoto Ramadhan Kambuga, na katibu CCM manispaa Janeth Kayanda |
![]() |
Waandishi wa habari wawapo kazini ofisini CCM |
Kamati ya
siasa ya halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi wilaya Bukoba, imelaani na ombi
la friends of Bukoba kwa waziri mkuu.
Akizungumza
na waandishi wa habari mkoani KAGERA, katibu mwenezi CCM manispaa ya Bukoba
Bwana RAMADHAN KAMBUGA, amesema kuwa kamati ya siasa ya wilaya kupityia kikao
chake cha 6/6/ 2014, ilijadili kwa kina ombi la Friends of Bukoba kwa waziri
mkuu, kumwomba avunje baraza la madiwani wa manispaa ya Bukoba.
Amesema kuwa
pendekezo lao kwa waziri mkuu, linalengo la kufifisha maendeleo ya wananchi
kwani halilengi kuleta usuruhishi ambao unatafutwa na serikali inayofuata mfumo
wa Demokrasia,
KAMATI YA
ccm WILAYA Bukoba, imesema kuwa ingekuwa tayari kuwaunga mkono FRIENDS OF
BUKOBA, kama wangetambua na kusimamia masuala ya ardhi, na kama wangesimamia
utekelezaji ushauri uliomo kwenye taarifa ya CAG, wakiongeza kuwa
hawakuwashirikisha wananchi kujua mapendekezo yao.
Hatahivyo
wameongeza kuwa Frieds of Bukoba, hawajawahi kujitambulisha wala kushughulikia
mgogoro wanaoutaja, hivyo chama kinashangazwa na kauli yao ya kuomba kuvunjwa
kwa baraza.
Wiki
iliyopita, wanaumoja wazawa wa Kagera waishio mikoani na nje ya nchi,
walimwandikia waziri mkuu barua kuomba avunje baraza la madiwani, katika
kipindi ambacho waziri mkuu alikwishatamka kuwa kufukuza madiwani siyo utatuzi
wa mgogoro wa Bukoba.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment