MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 4 June 2014

WANANCHI DODOMA WAHIMIZWA KUJIUNGA NA MIFUKO YA HIFADHI.



Wananchi  wameendelea kuhimizwa kujiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii pamoja na kuunda  vikundi kwaajili ya kupata mikopo mbalimbali.

Hayo yamesemwa na Naibu waziri wa kazi na ajira Mh. Makongoro  Mahanga nakusema kuwa serikari iko katika mchakato wa kuainisha vikokotoo kwa ajili ya ulinganisho wa gharama za michango ya wanachama katika mifuko hiyo ili kuweka usawa katika mifuko hiyo na kuifanya kuwa endelevu.

Pia amesema kwa sasa serikali bado inaendelea kutoa mikopo kwa wanachama kupitia vikundi mbalimbali ambapo amesema bado kuna mchakato wa kuangalia uwezekano wa kutoa mikopo kwa mtu mmoja mmoja.
Na Mwanaharakati.

No comments: