
Devotha alisema akifariki
asinunuliwe jeneza la kifahari, bali lichongwe kwa mbao za kawaida na lisiwekwe
mapambo yoyote, watu wasilie msibani kwake na kwamba endapo vitu hivyo
vitakiukwa, basi mwili wake utagoma kubebeka.
“Unajua duniani nimekuja uchi, sasa
siku nikifa sitaki mbwembwe za kununuliwa jeneza la mamilioni wakati nimeacha
watoto, ni bora hizo fedha wapewe wanangu ziwasaidie, vivyo hivyo pia sitaki
watu walie kwa kuomboleza kwenye msiba wangu kwa sababu watakuwa wananiumiza
tu, hata watoto na ndugu zangu nilishawaambia,” alisema Devotha.
Katika misiba ya hivi karibuni ya wasanii nyota,
imeshuhudiwa kamati mbalimbali zikiundwa na kuchangisha fedha nyingi ambazo
zimekuwa zikitumika kununulia majeneza ya bei mbaya, vyakula vya gharama na
shughuli zingine ikiwemo ukodishaji wa magari ya kusindikiza msafara wakati wa
mazishi.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment