
Bwana Lawa amesema kuwa blog ni kama
chombo kingine cha ahabari, hivyo taarifa zake zinatakiwa kuhaririwa kupitia
misingi ya habari, akisistiza kuwa wahariri wake kwa kiasi kikubwa, wanakosea kuweka
caption za picha ambazo zimekuwa zina makosa ya kisarufi na tahajia (spellings
jambo ambalo linapunguza ladha ya habari na taarifa mnazo post kwenye blog.
“Kutokana na hali hiyo ninawaomba
sana tena sana muimarishe uhariri wa habari hizo na hata pale mnapogundua
kuwapo kwa tatizo hata kama habari tayari imekwisha pandishwa yaani up-loaded
basi ishusheni ili ifanyiwe masahihisho” alisema Lawa.
Kwa upande wao waandishi na wamiliki
wa blog, wamekiri kupokea ushauri huo wa mtaalamu wa habari ambaye ahatahivyo
amekuwa mshauri mkubwa wa vyombo vya habari, baada ya kushika nyadhifa
mbalimbali katika vyombo vya habari, ikiwa ni pamoja na kuwa mkrugenzi
Kasibante fm redio Bukoba.
Hatahivyo waandishi wameomba MCT kuwapa mafunzo zaidi kuhusu kuandaa habari za blog, kwani wengi hawana ujuzi wa kutosha katika hilo.
Na Mwanaharakati.
Hatahivyo waandishi wameomba MCT kuwapa mafunzo zaidi kuhusu kuandaa habari za blog, kwani wengi hawana ujuzi wa kutosha katika hilo.
No comments:
Post a Comment