MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 5 June 2014

MFUMO UNAOTUMIKA KUKAGUA MAGARI BARABARANI KUTOPUNGUZA AJALI NA UNAONGEZA MIANYA YA RUSHWA.


Hali hii inashuudiwa mara kwa mara katika vituo vidogo na vya dharura kwenye barabara kuu kote nchini.
 

 Mwandishi wa mtandao huu, ameshuudia vitendo hivyo katika barabara ya Dodoma- Mwanza, ambapo katika maeneo ya Ikungi Singida, askari wa usalama barabarani walisimamisha basi la kampuni jina linahifadhiwa na kuzungumza na watumishi wake pembeni huku wakisikika wakicheka na baada ya hapo askari polisi aliyeonekana kuwa V tatu ambaye kijeshi anajulikana kama SAJENTI (SAGIN ) aliingia kwenye gari akiwauliza abiria kama wamefunga mikanda baadhi ya abiria walijibu kuwa gari halina mikanda, lakini akari huyo aliondoka pasipokujibu chochote.

 Katika mkoa wa Shinyanga karibu na chuo cha VETA, askari wa usalama barabarani alisimamisha basi hilo, na kumuita Kondakta ashuke na baada ya hapo walifokeana na badaye wakaanza kucheka huku askari akionekana anaandika jambo kwenye karatasi nyeupe ambayo Konda alitaka kuchukua mara ya kwanza askari akakataa na kurudisha mkono, mara ya pili akampa mkono kama anataka kuchukua karatasi lakini haikuwa hivyo na badala yake wakashikana na kuagana huku wakicheka, je aliandika ya nini kama hakiwa ya kusainiwa, na askari kushikana mkono na mtu ambaye wamefokeana na unaoonesha siyo wa salamu inamaana gani kwa jamii?

Na Mwanaharakati.

No comments: