MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 31 July 2014

NEWS ALERT!!! WATUMISHI WATANO WA HALMASHAURI WAFIKISHWA MAHAKAMANI

Ni watano wa Halimashauri ya wilaya ya Geita katika idara  ya misitu wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Geita baada ya kuwa na kutuhuma 30 likiwemo la kusababishia hasara kwa mwajiri wao kiasi cha shilingi milioni 22, 9866,400,


Akisoma mashitaka hayo mbele ya hakimu wa mahakama ya wilaya Desidery Kamgisha ,mwendesha mashitaka wa serikali Enosi Erasto alisema kuwa mnamo mwezi wa sita mwaka 2009 na mwezi wa 12 mwaka 2011 huko katika msitu wa akiba wa Geita,  kwa muda tofauti washitakiwa hao wakijua ni kosa la jinai na kwa makusudi   walitenda makosa hayo na kusabasha hasara kubwa kwa mwajiri wao.

Mwendesha mashitaka huyo ameongeza kuwa baada ya kutenda makosa hayo hawakuweza kutoa taarifa yoyote ya ukweli kwa mwajiri wao.

Aidha amewata watuhumiwa hao kuwa ni  Emanueli Mabala,Kasika Gamba,Elizakayo Yobu shuma, Alexanda Makali Masawe, Paulo Maganya, wote wakiwa ni watumishi  wa wilaya ya Geita.

Mara baada ya kusomewa mashitaka hayo kwa mara ya kwanza kwa hakimu Kamgisha  washitakiwa hawakujibu chochote kutokana na ushaidi kutomilika na wamerudishwa rumande baada ya kukosa vigezo vya dhamana na kesi yao itasikilizwa tena taree 07 mwezi wa nanae.

Na Mwanaharakati.

No comments: