MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 29 July 2014

RAIS ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI


Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Dkt. Parseko V. Ole Kone kuomboleza kifo cha aliyepata kuwa Naibu Waziri, Mbunge na Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Mheshimiwa Alhaji Mahami Rajab Kundya.
Mzee Kundya aliaga dunia jana, Jumapili, Julai 27, 2014 mjini Zanzibar.
Katika salamu zake, Rais Kikwete amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kuwa taifa limempoteza Mzee Kundya katika kipindi ambacho ushauri wake ulikuwa unahitajika sana na kuwa Watanzania wataendelea kumkumbuka kwa mchango wake katika nafasi zote alizozishikilia za Serikali, za Chama cha Mapinduzi na za kidini.
“Naungana nawe na wana-Singida wote katika kuomboleza kifo cha Mzee Kundya.Tumepoteza kiongozi ambaye mchango wake utaendelea kukumbukwa na sisi sote. Kupitia kwako, natuma pia salamu zangu za rambirambi kwa familia ya marehemu. Niko nao katika kuomboleza msiba huu mkubwa na naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu aiweke peponi roho ya Marehemu Mzee Kundya,” amesema Rais Kikwete.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
28 Julai,2014

Na Mwanaharakati.

No comments: