MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 21 September 2014

MARINE NA SUMATRA KAGERA WALALAMIKIWA KUFANYA HUJUMA WILAYANI MULEBA.



WADAU wa rasilimali za uvuvi  wilayani Muleba mkoani Kagera wamechanga kiasi cha Sh 40 mil kwa ajili ya kununua boti yenye mwendo kasi itakayotumika kukabiliana na vitendo vya ujambazi wa wavuvi ndani ya ziwa victoria.

Fedha hizo  zimechangwa jana wilayani humo  katika harambee iliyoongozwa na mkuu wa mkoa wa kagera kanali mstaafu Fabian Masawe na malengo ya wadau hao ni  kukamilisha Shilingi milioni  72  zinazohitajika kununua boti hiyo

Akisoma risala kwa wadau hao diwani wa kata ya Mazinga Bw Alex Thadeo amesema matukio ya ujambazi kwa wavuvi  wilayani Muleba yamewaathiri na mashine za uvuvi  65 zenye  thamani ya Sh292.5mil zimeporwa mwaka huu

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Muleba Bw Muhaji Bushako amelalamikia watumishi wa Marine na Sumatra mkoani Kagera kwa kuhujumu nguvu za wavuvi wanapoingia visiwani  bila wilaya kuwa na taarifa

Hata hivyo mkuu wa mkoa wa kagera Kanali mstaafu Fabian Masawe amewataka wavuvi kwa kushirikiana na vyombo vya dola kudhibiti vitendo  vya uvuvi haramu ili kuhakikisha samaki wanaovuliwa wanakuwa  ni wenye soko kiuchumi. 

Aidha amewaahidi wavuvi hao kuwapatia askari wa doria kutoka jeshi la polisi ambao watakuwa na mafunzo ya kutumia slaha kali kupambana na waharifu wanaovamia ziwani na kupora zana za uvuvi huku wakiacha madhara makubwa
 

Na Mwanaharakati.

No comments: