MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 7 September 2014

MWENYEKITI WA IPP AMUUNGA MKONO MBUNGE BUNGE BUKOBA MJINI



Waamini mkoani Kagera wameshauriwa kuwa makini wanapokuwa wanatamka maneno katika jamii ili kutunza amani na ulivu uliopo katika nchi yetu.

Kauli hiyo imetolewa na mchungaji wa usharika wa kanisa la kiinjili la kirutheli tanzania Kashura dayosisi ya kasikazini magharibi Alex Kasisi wakati akiongoza ibada maalum ya changizo la ukarabati wa kanisa hilo leo.

Mchungaji Kasisi amesema kuwa,ndoa nyingi zinazovinjika mara nyingi sababu inakuwa ni matumizi mabaya ya ulimi.

Katika haranbee hiyo Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Mheshimiwa Balozi Hamis  Kagasheki pichani juu, kwa niaba ya  Mwenyekiti wa Makampuni ya  IPP  Dokta REGNALD MENGI ametoa shilingi milioni kumi  ikiwa ni kuunga mkono jitihada za waamini katika ukarabati wa kanisa hilo kongwe la usharika..







Aidha katika harambee hiyo zimepatika shilingi milioni 22.9 ikiwa ni pesa taslimu na ahadi zilizotolewa na waamini na watu walioharikwa.
Ukarabati  wa kanisa hilo la Usharika wa kashura utagharimu shilingi milioni 15.2.

Na Mwanaharakati.

No comments: