MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 7 September 2014

NEWS ALERT!!! TANZANIA KUKABIRI MABADILIKO YA TABUIA NCHI NA MATAIFA JIRANI



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amerejea nchini jana kutoka visiwa vya Samoa ambako alimuwakilisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Mkutano wa Tatu wa Kimataifa kwa nchi za Visiwa.
 Katika hotuba yake kwenye mkutano huo Dk. Shein alisisitiza msimamo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuunga mkono malengo ya mkutano huo ambayo ni kuleta maendeleo endelevu katika nchi za visiwa kwa kuweka mkakati madhubuti kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi katika nchi hizo.

Alieleza pia haja ya ushirikiano thabiti na wa vitendo kutekeleza Malengo ya Milenia ambayo bado hayafikiwa katika kipindi cha ajenda ya maendeleo baada ya mwaka 2015.
 Aliwahakikishia wajumbe wa mkutano huo kuwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Viongozi wa Afrika kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi atasisitiza msimamo wa bara la Afrika katika mkutano ujao wa kilele kuhusu mabadiliko ya Tabaianchi unaotarajiwa kufanyika tarehe 23 Septemba 2014.

Akiwa visiwa vya Samoa, Dk. Shein alihudhuria pia uzinduzi wa Mpango wa Magharibi ya Bahari ya Hindi wa Changamoto za Ukanda wa Pwani na Mabadiliko ya Tabianchi ambapo aliuelezea mpango huo kuwa ni chombo muhimu katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi katika ukanda huo.
   
Dk. Shein alipata fursa ya kufanya mazungumzo kwa nyakati toafauti na Rais wa shelisheli Mheshimiwa James Michel na Rais wa Comoro Mheshimiwa  Ikililou Dhoinine.
Katika mazungumzo hayo viongozi hao walizungumzia suala la kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na nchi hizo.
 Mbali ya viongozi Dk. Shein alikutana pia na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Kimataifa cha Biashara (ITC) chenye makao yake mjini Geneva Uswizi ambapo Mkurugnezi huyo alimueleza Rais kuwa kituo chake kiko tayari kuisaidia Zanzibar kutekeleza mkakati wake wa kuongeza ajira kwa vijana na kinamama kwa kutumia rasilimali zilizopo Zanzibar.
 Katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Abeid Amani Karume Dk. Shein alipokelewa na viongozi mbali mbali wa chama na serikali wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi  na Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho.
 Miongoni mwa wajumbe waliofuatana na Dk. Shein ni pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Dk. Mahadhi Juma Maalim, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makanu wa Kwanza wa Rais Fatma Abulhabib Ferej na  Mshauri wa Rais Ushirikiano wa Kimataifa, Uchumi na Uwekezaji Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa
Wengine ni Kaimu Naibu Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Andy Mwandembwa, Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Sheha Mjaja Juma na mtaalamu wa mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Suleiman Kisimbo.
  Na Mwanaharakati.

No comments: