MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 7 September 2014

MAAJABU!!!DIWANI WA CCM AKAMATWA NA MATUNGURI GEITA.



POMOJA na Serikali kuendelea  kupiga marufuku kuwepo  kwa waganga wa kienyeji matapeli na wenye nia mbaya katika Nchi yetu ya Tanzania  bado suala hilo linazidi kupamba moto kwa kuibuka waganga hao katika Mkoa wa Geita.
                              Hayo yamebainishwa   baada ya  Diwani wa CCM  Mawazo Wiliam  wa kata ya Bugarama  Wilayani Geita Mkoani hapa kukamatwa akiwa na matunguri anayoyatumia kupiga ramli chonganishi yakiwa Nyumbani kwake anakoishi.

Wakiongea kwa Nyakati Tofauti baadhi ya wananchi wa kata hiyo kwa shariti la kutotaka kutajwa majina yao walisema kuwa Diwani huyo amekuwa akiwapigia Ramli chonganishi watu wanaokwenda kwake kwa ajili ya kupata tiba ya kienyeji hivyo kuwaomba wanaohusika kuchukua hatua dhidi ya Diwani huyo.

Wananchi hao wameongeza kuwa Diwani huyo amekuwa ni kero kwa watu kwani amekuwa akiwatapeli watu kwa kuwapatia Tiba za uwongo na kuwa chonganisha watu bila kuona kuwa yeye ni kiongozi.

Afisa mtendaji wa kata hiyo Juma Choba  alikiri kukamatwa kwa Diwani wake  lakini akasema kuwa  alikamatwa kwa tuhuma za kuwaosha wakataji wa mapanga  katika kata hiyo lakini akasema kuwa hajui kama ni kweli anafanya kazi hiyo kwani hajawahi kuona ila anasikia kutoka kwa wananchi kuwa diwani wake anawapigia ramli chonganishi.

Mimi nasikia kama wewe unavyosikia lakini sijawai kumuona ila amekamatwa yuko Polisi Wilayani inawezekana ni kweli kwa kweli siwezi kukataa alisema Mtendaji huyo.

Alipoulizwa Diwani Mawazo kuhusu kukamatwa kwake na kupiga ramli chonganishi alisema kuwa yeye ana lolote la kujibu juu ya hilo.

Jeshi la polisi  Mkoani hapa limethibitisha kukamatwa kwa Diwani Mawazo na uchunguzi unaendelea kubaini ukweli wa tukio hilo .


Na Mwanaharakati./Na. Valence Robert Geita.
 

No comments: