MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 18 September 2014

NEWS ALERT!!WANANCHI WALAANI MGAMBO KUMVUNJA MBAVU MWALIMU BILA KUKAMATWA GEITA.



MGAMBO wa kituo cha polisi cha Nzera kilichopo Tarafa ya Bugando Wilayani Geita Mkoa wa Geita wanatuhumiwa kumshambulia kwa kipigo mwalimu msitaafu kisha kumvunja mbavu zake bila kukamatwa

Kufuatia hali hiyo wananchi  wa kijiji cha Nyamboge Katika kata ya Katoma Wilayani Geita Mkoani hapa wamelituhumu  Jeshi la polis Mkoani hapa kwa kushindwa kumkamata mtuhumiwa aliyeusika kumpiga  Samsoni Mzingwa(58) na kumvunja mbavu zote na huku aliyefanya  kitendo hicho hakiwa mitahani hakitamba  na kujigamba kuwa polis wemewekwa mfukoni mwake.

Tukio hilo limetokea tarehe  14 mwaka huu majira ya asubuhi wakati  Mwalimu Samsoni Mzingwa(58),akielekea shambani kwake.

Akizungumza kwa shida Samsoni alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni yeye alikodiswa  shamba mwezi huu kwa ajili ya la kulima Maindi  na Rukasi Bunzali pamoja na Wiliamu Bunzali wote wakiwa ni wanafamilia moja kwa makubaliano ya kuwalipa miliono moja na laki tanona kulipa pesa zote  na kuanza kulima mala moja kwa ajili ya kupanda mazao yakiwemo maindi na mahalage.

Lakini juzi wakati akienda shambani kwake alishutukia watu wanne wakiwa na mgambo wawili wa kituo cha polis Nzera kilichopo katika wilaya Geita wanamzingila na kuanza kushushia kipigo kikubwa hadi kumvuja mbavu huku wakimtembeza uchi wa mnyama ali iliosababisha maumivu makali na kulazimika kulazwa katika Hospitali ya wilaya ya Geita.

Alisema kuwa pamoja na kuwatambua waliomfanyia kitendo hicho na kuwataja kwa majina kuwa ni Masalu Mwnangwa na Kona Mwanangwa lakini wamewakamata mgambo na kona wakati Masalu akizidi kutamba mitaani na huku polis wakiwa wanamuona lakini awataki kumkamata uenda wanamuogopa kwa kuwa ana pesa alisema Samson.

Naye Mtoto wa Mzee huyo aliyejitambulisha kwa jina la Baraka Samsoni alisema kuwa kuwa yeye alipata taalifa na kwenda kulipoti kwa OCS Nzera lakini akuna kilichofanyika zaidi ya kuzunguswa na OCS huyo huku akiambiwa asiwafundishe kazi asikali hao.

Mganga mfawidhi wa Hoaptali ya Wilaya ya Geita Adam Sijaona amekili kumpokea mgonjwa na kumalaza wodi No 8 na kusema baada ya kupiga Picha waliona  wanasubili majibu lakini vipimo vya awali vinaonyesha ameumia mbavu.

Kamanada wa Jeshi la polis Mkoani hapa Josefu Konyo alipopigiwa sm yake ya mkononi na mwandishi wa habali hizi na kutaka kujua kwanini awajamkamata mtuhumiwa alikata na alipotumiwa ujumbe mfupi zaidi ya mala mbili akujibu


Na VALENCE ROBERT,GEITA 
 
Na Mwanaharakati.

No comments: