MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 14 September 2014

NEWS ALERT!!!WANAOPORA MAENEO YA WACHIMBAJI WADOGO KUKIONA - GEITA.



Kauli hiyo imetolewa juzi na Mwenyekiti CCM Mkoa wa Geita Josefu Msukuma mbele ya Naibu waziri wa nishati na madini wakati akikabidhi eneo la kuchimba dhahabu kwa wachimbaji wadogo wadogo lililoko katika kijiji cha Lwamgasa Wilayani Geita mkoani humo.

Msukuma alisema kuwa kumekuwa watu ambao si waungwana wanaopora maenaeo ya wachimabaji wadogo wadogo kwa kuwalazimisha kuingia ubia na mwishowe wazudhulumiwa na kuwafukuza ambapo huanza kuhangaika.

Aliendelea kusema kuwa migogoro ya wachimbaji wakubwa na wadogo haiwezi kuisha kama wachimbaji wakubwa hawataacha kuwadhulumu maeneo yao hivyo kumuomba naibu waziri kuwachukulia hatua kali wote waliopora maeneo yaliyotengwa kwa wachimbaji wadogo wadogo na kujimilikisha wao.

Naye Naibu waziri wa nishati na madini akiongea na wananchi wakati wa kuzindua mgodi huo aliishukuru benki ya dunia na Mgodi wa GGM kwa kukubali kutoa pesa nyingi na vifaa kwa kuwasaidia wananchi hao mara baada ya kutambua mahusiano mazuri yaliopo kati ya mgodi na Serikali.

Vilevile aliwataka wananchi wa kijiji hicho pamoja na Serikali ya mkoa huo kusimamia vizuri mradi huo ili uwezi kuwaendeleza wakazi wa mkoa mzima kwa kuwanufaisha wao.

Mkurugenzi wa Geita Gold Mine Michael Anen alisema kuwa wataendelea kuwasaidia wanachi wa mkoa wa Geita kwa kuwa ni mahusiano mazuri yaliopo kati yao na Mgodi huo ambapo wanarudisha faida yao wanayoipata kwa wananchi wao.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: