Jonas akihojiwa na waandishi wa habari
kuhusiana na tukuo hilo muda mfupi baada ya tukio.
|
Mtoto wa Naibu Waziri wa zamani wa
Afya na Mbunge wa Morogoro kusini mashariki Lucy Nkya amewaambia waandishi wa
habari kwamba habari zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba amerushiana
risasi za moto na mama yake mzazi ofisini kwao mkoani Morogoro zimepotoshwa.
Jonas Nkya amesema kilichotokea
alipokwenda ofisini hapo kuchukua gari akitokea shambani na bastola ilidondoka
chini na ikajifyatua risasi moja na kuzua taharuki kwa watu.
“Kwanza mimi sina ugomvi wowote na
mama yangu mimi nilikua shamba narudi nashangaa nimezungukwa na waandishi wa
habari wakitaka kujua ukweli wa habari hizi”.
Mimi nashanga habari zilizozagaa
kwenye mitandao zimetokea wapi.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment