MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 20 October 2014

BREAKING NEWS!!! MTUHUMIWA NAMBA MOJA WA MABOMU NA TINDIKALI AUAWA KWA RISASI NA POLISI ARUSHA


Taarifa ya hivi punde kupitia moja ya redio hapa nchini, inasema kuwa Jeshi la polisi mkoani Arusha limemuua kwa kumpiga risasi mtuhumiwa namba moja wa milipuko ya mabomu katika mikusanyiko na kuwamwagia viongozi wa dini tindikali, baada ya kujaribu kutoroka akiwa chini ya ulinzi njiani kwenda kuonyesha bomu alilokuwa amelificha maeneo ya kondoa mkoani Dodoma .

Taarifa iliyonifikia memtaja mtuhumiwa huyo anayetajwa kuwa namba moja wa kesi ya ulipuaji mabomu jijini Arusha, kuwa ni Yahaya Hassan Omar kwa kupigwa risasi na askari wa jeshi la polisi wakati alipojaribu kutoroka akiwa chini ya ulinzi.

Mtuhumiwa huyo, ameuawa zikiwa zimepita siku chache baada ya kuuawa kwa mtu mmojamkoani Arusha aliyekuwa akituhumiwa kuwateka na kuwauawa wananwake mbalimbali mkoani humo
 

Na Mwanaharakati.

No comments: