MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 14 October 2014

BREAKING NEWS!!!ASKOFU KILAINI; NYERERE ALIWEKA USAWA KATIKA MASUALA YA DINI NA KIJAMII.

Baba askofu Kilaini akizungumza na mwandishi Mac Ngaiza, katika makaazi yake Bunena Bukoba mjini.



“katika shughuli za kijamii, watu wanapotoka katikabaadhi ya taratibu kuwa kitu Fulani kinazuiliwa lakini ngoja tufanye kidogo, tofauti na dini inayoagiza kuwa hata kujaribu ni kosa, hayo ndiyo mambo Mwalimu alizingatia” amesema Kilaini.

Amesema kuwa mambo yanayomsikitisha zaidi, ni kuendelea kutumia jina lake kwa uongo huku mambo ambayo yalianzishwa naye wakati huo yakichakaa na viongozi wakiendelea kuyatumiahuku yakiwaumiza watanzania, akitolea mfano wa meli ya Mv Victoria,ambayo amesema mpaka sasa ina zaidi ya miaka 60, hivyo imechakaa na inaendelea kuwasumbua watanzania hasa wakaazi wa mkoani Kagera, ambao tangu awali waliamini usafriri huo na uliwasaidia, lakini viongozi wameziba m,asikio kufanya utaratibu katikahilo.

Amesema melihiyo zamani ilikuwa ikifika ukoba sa 12 alfajiri kutokea Mwanza, lakini sasa anaisikia saa 3 asubuhi, kuwa hicho ni kiashiria kuwa ina matatizo makubwa na ikiendelea kufanyiwa mzaha itapoteza watanzania wengine katama ilivyotokea 1996.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: