Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la
soka nchi TFF, imemfungia wakili Damas Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka
kwa muda wa miaka saba.


Ndumbaro ambaye aliingia katika
mzozo mkubwa na rais wa TFF, Ndugu, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF
kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa
klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya
Tanzania Bara, na Azam Tv.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa Shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu. Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia, Bodi ya Ligi amekanwa ‘ hadharani’ na vilabu huku vikisema kuwa ‘ havikumtuma’ kuzungumza yale ambayo alisema mbele ya vyombo vya habari. Klabu zimesema alizungumza kwa ‘ utashi’ wake mwenyewe, na si wao walimtuma.
‘ Kilichomuhuku’ ni yeye kutaka kubadilisha maamuzi ya kamati ya utendaji ya TFF bila kuthibitishwa na wajumbe wa Bodi ya Ligi na kukubaliana. Kupingana maamuzi ya kamati ya utendaji ni kosa la kinidhamu.
Ndumbaro amehukumiwa kutokana
na makosa hayo na kama angezungumza kwa niaba ya klabu basi adhabu hiyo
ingekwenda kwa kwao, lakini yeye alijizungumzia tu kama vile alivyotaka iwe.
Na:shaffihdauda.com
No comments:
Post a Comment