
“Habari za jioni Watanzania wenzangu, kutokana na kuwa
nimekuwa nikisemwa sana, maneno mengi yasio na tija juu ya hili taji la U-Miss
anzania 2014,,mpaka kupelekea nisiwe na amani na uhuru ndani ya nchi yangu
Tanzania, kwa roho safi nimeamua mwenyewe kujivua taji hilo na kuacha wanaye
ona anastahili taji hili apewe ili niendelee na maisha yangu kwa amani ,isiwe
shida sana kwani sitegemei taji hili ili kuishi!!” imeandikwa katika ukurasa
huo.
Akizungumzia uvumi huo, Lundenga alisema hakuna ukweli juu
ya taarifa hiyo, na kwamba kama lingekuwa na ukweli ni wazi kwamba Sitti
angeiarifu kampuni yake, inayoratibu kinyang’anyiro hicho kilichotimiza miaka
20 mwaka huu.
“Hakuna taarifa iliyotufikia hadi sasa kuhusiana na taarifa
hizo. Sitti anajua anapaswa kufanya nini kama anaamua kulitema taji, ambapo
anapaswa kutuarifu sisi kabla ya kuripoti hilo mahali popote. Kwa kuwa
hajafanya hivyo, tunaamini hilo halipo nab ado tunamtambua kuwa mrembo wetu,”
alisema Lundenga.
Kwa upande wa mama wa mrembo huyo, alisema ameshtushwa na
taarifa za mwanaye kujiuzulu na kusema si za kweli, kwani kama angepanga
kufanya hivyo asingefanya kwa kificho, badala yake angeitisha mkutao na
wanahabari: “Hawezi kujiuzulu kienyeji hivyo na hata mimi mama yake sina
taarifa hizo, hayo ni matumizi mabaya ya mitandao.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment