MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 14 October 2014

NEWS ALERT!!! WABUNGE WA KAGERA WACHARUKIA SERIKALI KUSIMAMISHA MELI YA MV VICTORIA

Ni baada ya matatizo yanayoisibu meli hiyo na kuzua wasiwasi kwa abiria, huku wakisisitiza rais kutimiza ahadi.



Baadhi ya wabunge wa mkoani Kagera wameiomba serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, kusimamisha meli ya MV VICTORIA kuendelea na safari zake kati ya Mwanza na Bukoba mpaka ifanyiwe matengenezo, au iletwe nyingine.

Akizungumza kwa niaba ya wabunge hao, Mbunge wa jimbo la Muleba Kaskazini, CHARLES MWIJAGE amesema kuwa  haiwezekani  kuona meli hiyo ambayo inatia shaka kuendelea kusafirisha watu.

Bwana Mwijage amewaomba wananchi kuwa wavumilivu,  wakati wabunge  hao wakishirikiana  katika  kufuatilia ahadi ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Kikwete  ya kununua meli mpya.

Mwishoni mwa wiki,  abiria 381 waliokuwa wanasafiri na meli ya MV Victoria, kutoka Bukoba kwenda Mwanza,  walikumbwa na hofu baada ya mfumo wa kuendesha meli hiyo  kushindwa kufanya kazi  ikiwa majini.

Meli hiyo iliyoondoka katika bandari ya Bukoba Ijumaa usiku,   mfuko wake wa kuendeshea meli ulishindwa, ikiwa zimebakia maili kadhaa kabla ya kufika katika bandari ya Kemondo.

Na Mwanaharakati.

No comments: