MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 9 October 2014

NEWS ALERT!!! WALIOVAMIA ENEO LA MWEKEZAJI WAONDOKE MARA MOJA GEITA



WANANCHI waliovamia Eneo la Nyantorotoro lililoko katika kata ya Kalangalala wilayani Geita Mkoani humo, wametakiwa kuondoka mara moja katika eneo hilo ili kumpisha muwekezaji mwenye leseni kuendeleza shughuli zake za kuponda kokoto.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa madini wa mkoa wa Geita Eng. Pius R. Lobe wakati akiongea na wananchi hao mara baada ya muwekezaji huyo Majaliwa Maziku kulalamika kwa kusimama kwa shuguli zake baada ya wananchi wa maeneo mbalimbali ya mji wa Geita kuvamia na kuanza kuponda kokoto katika eneo lake.

Pius alisema kuwa mwekezaji huyo ana leseni kumi ambazo zimesajililiwa kisheria na analipia mapato makubwa serikalini na kwamba wananchi hao wanaoponda kokoto ni wavamizi wanatakiwa kuondoka mara moja kwani walishalipwa mda mrefu lakini waligoma kuondoka kutokana na maneno ya baadhi ya wanasiasa.

Jamani mnatakiwa kuondoka mara moja kwani mwekezaji huyo ana leseni kisheria na mkiendelea kukaa hapa mtakamatwa na mtafikishwa mahakani hatutaki kutumia nguvu, aliseama Pius.

Naye muwekezaji huyo Majali Maziku aliwatafutia Eneo lingine wananchi hoa ili wasiendelee kuhangaika ila wengine walikwenda lakini wengine waligoma jambo ambalo limemsababishia hasala kubwa kutokana na wavamizi hao kuiba vifaa vya baadha ya mashine zake.

Wananchi hao walikubali kuondoka na kuongeza kuwa kumekuwa na wanasiasa ambao wamekuwa wakiwachangisha pesa na kuwaambia kuwa mwekezaji huyo hana haki kumbe ulikuwa na uongo na kumuomba mwekezaji huyo kuwapatia ajira wananchi wa kijiji hicho.

Jamani tumekubali kuondoka kumbe tulidanganywa na viongozi ambao si wazuri sisi tunakuomba utupatie ajirajapo tulikuchelewesha kufanya kazi alisema Juma.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: