MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 28 October 2014

NEWS ALERT!!! WATALAAMU WAPAMBANA NA TATIZO LA NJAA KAGERA

 Wakati huo huo wakulima wameshauriwa kutumia mbolea aina ya CAN kutokana na mikoa ya kanda ya ziwa kuwa na kiwango cha juu cha mvua ambayo huondoa Nitrogen kwenye mbolea hiyo, ambapo pia matumizi ya samadi yaendane na utegenezaji na utunzaji mzuriwa samadi hiyo kuanzia chakula anachokula mfugo, bada la kuhifadhia mbole pamoja na kuweka shambani kwa wakati.

 Pia jambo la mnyororo wa thamani limezungumzwa, katika kuhakikisha mazao yanayozalishwa hasa viazi lishe ambavyo vinatoa matunda mengi, kuviwekea mpango wa uzalishaji, usindikaji na uzaaji kupitia mnyororo huo wa thamani.


Moja ya makundi ambayo yameshapata faida ya matumizi sahihi ya mnoyororo wa thamani ni kikundi cha BUHEA ambacho ni cha wakina mama katikamanispaa ya Bukoba wanaozalisha unga, maziwa na bidhaa nyingine za viazi lishe na Soya.
                                     

Na Mwanaharakati.

No comments: