MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 18 October 2014

UZINDUZI WA CHANJO MANISPAA YA BUKOBA, MWAMKO BADO UKO CHINI







Mratibu wa Chanjo  Mkoa wa Kagera,  DEOCLES MJWAHUZI  amesema  kuwa mwaka 2013   Watoto Elfu  72   na  611  walitegemewa kupata chanjo hiyo,  lakini watoto waliochanjwa ni watoto  elfu 35 na 979,  ambapo ni pungufu  na matarajio.

Amesema kuwa ili kufikia malengo ya idadi inayotakiwa kuchanjwa na kuepusha tatizo la mwaka jana, wazazi na walezi wote wenye watoto kuanzia  miezi tisa hadi  miaka 15 wanatakiwa kupeleka watoto wao ili kupatiwa chanjo hiyo.

Ameongeza kuwa katika chanjo hiyo,   watoto laki nne  na elfu 71 na 214 watapatiwa dawa ya Vitamin A ambapo watoto laki nne na elfu 18 na  857 watapatiwa dawa ya minyoo.

Bwana MJWAHUZI   amesema watoto watakaochanjwa  watakuwa na alama  ya muda kwenye kidole kidogo cha mkono wa kushoto,  na kuwa watoto ambao  hatakuwa na alama hiyo wazazi na walezi wao watachukuliwa hatua za kisheria.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: