MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 25 November 2014

NEWS ALERT!!!MDAHALO WA WARIOBA ULIOVURUGIKA UNAENDELEA SASA HIVI

Jaj Warioba katika mdahalo unaoendelea, amesema kuwa bunge limepoteza mwelekeo na kuingilia mambo ya serikali, ambapo ametolea mfano bunge kuagiza polisi kukamata wanaokiuka masuala ya utekelezaji.


Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imeandaa mdahalo huo maalumu wa Katiba kwenye Ukumbi wa Mlimani City ambao mzungumzaji mkuu ni Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
 
Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Joseph Butiku amesema kwamba mdahalo huu wa amani ni kwa ajili ya Watanzania wenye mapenzi mema na ukowazi, ikiwa ni sehemu ya kuziba pengo la mdahalo wa Katiba uliovunjika Novemba 2 ambao ulifanyika kwenye Hoteli ya Blue Pearl.
 
Ulivunjika baada ya kutokea vurugu zinazodaiwa kuanzishwa na kikundi cha watu kwa lengo la kuvuruga uwasilishwaji wa ujumbe wa Katiba, huku Katibu wa Uhamasishaji wa UVCCM, Paul Makonda akitajwa kinara wa vurugu hizo.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: