MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 25 December 2014

BREAKING NEWS!!! SAKATA LA MELI MV VICTORIA UBADHILIFU WABAINIKA UONGOZI WATIMULIWA WENGINE WAWEKWA KIPORO



Kutokana na meli ya Mv Victoria kukwama safari zake mara kwa mara na kuzua mjadala na hasara kwa abiria na wafanyabiashara, waziri wa uchukuzi HARISON MWAKYEMBE atimua uongozi mzima bandarini hapo na kuteua wapya.
Waliofukuzwa kazi ni Meneja mkuu Projest Kaija, na nafasi yake imechukuliwa na Fabian Mayenga.
Kaimu mhasibu mkuu Tito W.Mwambagi, nafasi yake kuchukuliwa na Beatus R. Rugalabamu, kaimu meneja masoko biashara, ameondolewa Cpt Obeid Nkongoki nafasi yake inachukuliwa na Cpt Winton Mwasa.

Aliyefukuzwa mwingine ni kaimu meneja wa tawi Mwanza Beatus T. Mghamba na kuingia Bwana Philemoni Bagambilana, Kaimu tawi Kigoma ameondolewa Bwana Abel Giliard na nafasi yake kuchukuliwa na Anthony Stephen, huku kaimu mwanasheria na menejautumishi anakuwa Fabian Mayenga baada ya kuondolewa Josephat Mshumbusi .

Meli hiyo imesimamishwa kutoa huduma ili ifanyiwe ukarabati wa kina, baada ya kubainika kuwa uongozi uliokuwapo ulikuwa ukiweka spare fake, na kusababisha adha kubwa kwa watumiaji.

Waliopewa onyo sima kwenye picha hii chini.
 
Uongozi mpya umeanza kazi tangu tarehe 18 Dec 2014.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: