Katika mkutano wake uliofanyika (juzi)kwenye uwanja wa soko la mtaa wa mkoani mjini Geita,uliokuwa
uhutubiwe na mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Geita Vicky Kamata kabla ya kushindwa kufika,baadhi ya viongozi wa chama hicho walijikuta wakiwa peke yao na
wanachama wao wachache wenye sare za chama hicho.
Wakizungumza kwa
nyakati tofauti baadhi ya wananchi wa mtaa wa mkoani waliokutwa wakifanya
shughuli zao bila kusogea katika mkutano huo walidai kuwa hawaoni sababu ya
kuwasikiliza wanaCCM kwa kuwa Rais Kikwete haoneshi nia ya dhati kuwawajibisha
watuhumiwa wa Escrow.
''Ndugu yangu kwa hali ilivyo hapa
nchini tumeamua hata tusihudhulie mikutano yao kabisa hawa watu ili
wajifunze,yaani safari hii ni bora tuchague jiwe kutoka chama kingine na si
chama cha mapinduzi,tumechoka kaka’’alisema Mabula kaloli mkazi wa mtaa wa
mkoani aliyekutwa akicheza karata na wenzake umbali wa zaidi ya mita 300 kutoka
eneo la mkutano.
Mwingine ni Mayala Kubingwa aliyedai
kuwa,wakati nchi inatimiza miaka 53 ya uhuru wa kutokuwa na uhuru hakuna
mtanzania hususani wa Geita anayeweza kusherehekea miaka hiyo,wakati hakuna
huduma za kijamii na kudai kuwa iwapo chama hicho kingekuwa na nia ya
kuwakomboa watanzania kingenyonga mafisadi wote wa Escrow.
No comments:
Post a Comment