MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 1 December 2014

SIKU YA UKIMWI DUNIANI; KAGERA WAJISAHAU, NJOMBE SASA KUFANYA TOHARA


Ugonjwa huo ulianzia  mkoani Kagera mwaka 1983 wilayani Misenyi katika kata ya Kanyigo, ambapo Wananchi mkoani Kagera wanaadhimisha siku hiyo huku kiwango cha ugonjwa huo kikionesha kupanda hadi 4.8% mkoani humo,kutokana na sababu zilizotanjwa kuwa wamejisahau baada ya mashirika na taasisi kwa kushirikiana na wananchi kukomesha UKIMWI miaka ya nyuma kufikia 2010.

Pamoja na wananchi kujisahau kuwa UKIMWI ulikwisha mkoani Kagera, uwapo wa visiwa vinavyozunguka mkoa huo katika ziwa Victoria vya Nyabesia, Nyaburo, Kerebe, na Bumbire, umechangia kuongezeka kwa UKIMWI kutokana na wanaokwenda kutafuta pesa kwa kujiuza kama alivyofafanua afisa ustawi wa jamii mkoani Kagera


Mratibu wa UKIMWI mkoani Kagera kupitia taasisi ya kupambana na kudhibiti UKIMWI, Bi Jeneviva Emmanuel amesema kuwa TACAIDS kwasasa  imeamua kushirikisha asasi mbalimbali za serikali na zisizo za kiserikali ili kuona kama itaweza kukabiliana na kuanza kupanda kwa kiwango hicho cha maambukizi, akitaja wakati wa miaka ya themanini kuwa kiwango cha maambukizi kilifikia 19% ambapo jitihada zilizofanywa na wahisani zilipunguza maambukizi hayo hadi 3.4% kufikia mwaka 2011.



Na Eddy Blog, Njombe
Wananchi mkoani Njombe wameaswa kutoliingiza suala la tohara ya wanaume na imani za dini kwa kuwa suala hilo ni kwa ajili ya kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI na manufaa mengine ya kiafya na si vinginevyo

Hayo yamebainika wakati wa uchangiaji mada iliyowasilishwa katika kikao cha wadau wa mapambano dhidi ya vvu kilichoandaliwa na tume ya taifa ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) ambapo imeonekana miongoni mwa changamoto ambayo shirika la JHPIEGO lilikutana nayo wakati wa utekelezaji wa huduma ya tohara ya wanaume ni imani ya dini

Mmoja wa wachangiaji hao askofu mstaafu Dkt Peter Lukumbusho Mwamasika ameeleza kuwa wapo baadhi ya watu wanadai wanaume wakifanyiwa tohara wanakuwa wamehamishwa katika imani yao ya kikristo na kupelekwa katika imani ya kiislamu jambo ambalo limepingwa vikali kuwa halina ukweli wowote

Askofu huyo amesema katika kipindi hiki ambacho kila mmoja anapambana na maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi, tohara imegundulika kuwa ni moja ya njia inayopunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa waliofanyiwa tohara hivyo mwanaume aliyefanyiwa tohara imani yake ya dini inabakia pale pale

Kwa upande wake mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya Bunge inayoshughulikia Ukimwi Mh. Lediana Mng'ong'o amewataka viongozi wa siasa kushirikishwa katika jitihada za kupambana na maambukizi ya VVU

"Humu ndani siwaoni madiwani, siwaoni wenyeviti wa halmashauri, angalau nawaona wakuu wa wilaya, wenyeviti wa halmashauri ndio wasimamizi wa sheria ndogondogo ninaomba tuwashirikishe sana maana wanaushawishi mkubwa katika hili" amesema Mng'ong'o

Amesema kwa nafasi hii wakishirikishwa viongozi wa siasa watakuwa wanapeleka taarifa hizo kwa wapiga kura wao suala hilo litasaidia kuwa na mabadiliko makubwa katika jamii  


Maadhimishoya siku ya UKIMWI Duniani,kimkoa yanafanyika wilayani Biharamulo, kitaifa yanafanyika mkoani Njombe,  ambao unaongoza kwa maambukizi kitaifa kwa asilimia 14.8 huku Pemba ikiwa chini ya asilimia 1.
Na Mwanaharakati.

No comments: